Select Menu

Ads

Random Posts

Powered by Blogger.

Design

Technology

Circle Gallery

Shooting

Racing

News

Bottom

Wednesday, July 2, 2014

Professor Jay aongea na COSOTA kuhusu utaratibu wa redio na TV kuwalipa wasanii kwa kucheza kazi zao

Msanii wa Hip Hop,Joseph Haule aka Professor Jay jana alikitembelea chama cha Haki Miliki Tanzania ‘COSOTA’ na kuwauliza kwanini Radio na TV za Tanzania haziwalipi wasanii pindi wanapoziga nyimbo za wasanii kwenye vituo vyao.

Akizungumza na Bongo 5,Professor Jay alisema kuwa baada ya kupeleka shauri hilo, wahusika ambao ni COSOTA wamesema wapo kwenye vikao kulijadili.

“COSOTA sio watu wa mwisho , wameniambia kuna vikao vingine vinaendelea ,tuweke subira lakini hili suala linajadiliwa kila siku. Lakini tuseme kweli haya mambo yanatakiwa yaanze ingawa kumekuwa na changamoto , hata wasanii wenyewe wanafanya muziki kama muziki ilimradi wanajifurahisha lakini kama watakuwa serious vyombo vya habari ‘Radio na Tv’ zinawalipa watu maana yake hata wasanii wenyewe watakuwa serious kufanya muziki kuwa perfect na itachuja upi mchele zipi pumba, naamini hivyo vyombo haviwezi kukubali kumlipa mtu ambaye yupo shaghalabaghala ambao hawafanyi muziki unaoeleweka,” alisema Professor.