Select Menu

Ads

Random Posts

Powered by Blogger.

Design

Technology

Circle Gallery

Shooting

Racing

News

Bottom

Thursday, July 24, 2014

Video: Mashabiki wa Palestina wavamia mchezo wa Macabi Haifa ya Israel

Mchezo wa kirafiki kati ya klabu ya Lille ya nchini Ufaransa dhidi ya Macabi Haifa uliochezwa nchini Uturuki, umeingia dosari baada ya kundi la mashabiki waliokuwa wamebeba bendera ya Palestina kuingia uwanjani.

Kitendo hicho ambacho kilizua vurugu kwa dakika kadhaa, kilijitokeza datika dakika ya 84 ya mchezo ambapo katika hali ya kushtukiza mashabiki hao walijitosa uwanjani pasina uwoga wowote.

Mbali na kundi la watu kuingia uwanjani, picha za televisheni zilimuonyesha mmoja wa wavamizi hao wa uwanja akipigana na mchezaji wa klabu ya Macabi Haifa, kitendo ambacho kimeashiria tofauti zilizopo kati ya Palestina na Israel.
Hata hivyo klabu ya Maccabi Haifa ina historia kubwa ya kuwa na wachezaji wengi kutoka nchi za kiarabu kama Taleb Tawatha, Mohammadou Idrissou, Weaam Amasha, Ataa Jaber, Mohammed Kalibat pamoja na Ismaeel Ryan.