Select Menu

Ads

Random Posts

Powered by Blogger.

Design

Technology

Circle Gallery

Shooting

Racing

News

Bottom

Monday, July 14, 2014

Video: Producer Mensen Selecta aeleza kuwa hayupo kwaajili ya wasanii wa Arusha tu

PRODYUZA anayefanya vizuri kwa sasa hapa nchini katika utayarishaji wa muziki wa kizazi kipya, Mensen Selecta kutoka Studio ya D Fatality, amekanusha uvumi unaozidi kutanda kuhusiana na kuwabeba wasanii kutoka Arusha ili ‘kuwaboost’ na kuwaweka juu kwenye ‘game’.

Akizungumza kupitia Global TV Online, Selecta amesema kufanya kazi na wasanii kutoka mkoani humo haimaanishi kuwa yupo kwa ajili ya wasanii kutoka mkoa huo, bali anafanya nao kazi kwa kigezo cha kuangalia kipaji.

Arusha mimi ni nyumbani kwangu lakini haimaanishi kuwa nipo kwa ajili ya wasanii kutoka huko, kwa kifupi mimi naangalia kipaji cha msanii na siyo kumbeba mtu,” alisema Mensen.