Picha ya Kim Kardashian ya mwaka 2010, aliyoituma kwenye ukurasa wake wa instagram kabla Baby North hajazaliwa. |
Katika ukurasa wake wa Instagram Kim alituma picha ya mwaka 2010 ikimuonyesha umbo lake kipindi alivyokuwa mwembamba.
Katika picha hiyo aliambatanisha maneno yafuatayo; ‘Throwback to a few years ago#skinnyDays’.
Hata hivyo staa huyo maarufu kama Mrs. West yupo katika diet pamoja na ratiba ya mazoezi ya mwili ili kuhakikisha anapunguza uzito alioupata baada ya kujifungua ili kurejea katika umbo lake la mwanzo lililokuwa likikosha nafsi za wengi.