Select Menu

Ads

Random Posts

Powered by Blogger.

Design

Technology

Circle Gallery

Shooting

Racing

News

Bottom

Wednesday, July 16, 2014

Apania kuanzisha nchi ya kifalme Afrika, kutimiza amri ya bintiye

Mwanamme mmoja kutoka Marekani amedai umiliki wa kipande kidogo cha ardhi barani Afrika kama ufalme wake kwa sababu bintiye anataka kuwa binti mfalme  

Jeremy Heaton aliambia BBC kuwa amesafiri kutoka Virginia nchini Marekani na bendera yake kutangaza eneo hilo kwa Ufalme wa ‘Sudan Kaskazini’,  eneo hilo ni jangwa la mraba wa maili 800 lililo kati ya Misri na Sudan, na halijamilikiwa na nchi yoyote Alisema kuwa ameandikisha rasmi maombi kwa nchi hizo mbili, japo bado hajapata  jibu

Princess Emily akiwa amevaa tiara
‘Princess Emily’ huvalia tiara kila mahali anapokwenda kuashiria kuwa yeye ni mwanamfalme , bwana Heaton aliarifu BBC kuwa bintiye, Emily, aliuliza kwa sauti isiyo ya mzaha iwapo siku moja angekuwa binti mfalme ‘Kama babake, nilitambua kuwa ombi lake halikuwa mzaha, Heaton alisema. Nilitafiti vipande vya ardhi visivyomilikiwa na nikabahatika kuvigundua.’   

Ili kuadhimisha miaka saba tangu kuzaliwa kwa bintiye, Heaton alisafiri kwenda panapofahamika na wenyeji kama ‘Bir Tawil’ ili kutimiza ombi la Emily

Picha  ikionyesha kipande cha ardhi cha Bir Tawil  kinachotakiwa na Bwana Jeremy Heaton ili aweze kukitawala kama mfalme wa eneo hilo
Heaton ambaye ana watoto watatu alisema kuwa angefanya lolote ili kudhibitishia wanawe kuwa anaweza kuenda kokote kwa ajili yao ambapo tarehe 16, mwezi Juni, Heaton aliwasili jangwani na kuweka bendera iliyochorwa na bintiye, na kusisitiza madai yake ni halali       

Alidai kuwa kwa miaka mingi nchi kadhaa, ikiwemo Marekani, zilidai umiliki wa ardhi kwa kuweka bendera kwenye ardhi hiyo. Sasa bwana Heaton anasema atajaribu kuomba usaidizi kutoka kwa Umoja wa Afrika (AU)   

Mzozo wa mipaka kati ya nchi ya Sudan na Misri unaashiria kuwa jangwa hilo ni kati ya vipande vya mwisho duniani visivyomilikiwa,  tofauti, anavyosema, ni kuwa aghalabu vita huzuka ili kupata umiliki huo, bali kwa kesi yake, kuanzisha nchi hiyo ni ishara ya mapenzi yake kwa bintiye      

Hata kama hakuna uwezekano kuwa Jeremy Heaton atakuwa mfalme wa nchi hiyo mpya ya Sudan kaskazini, ana mipango atakavyoendeleza nchi hiyo

Binti mfalme Emily, aitwavyo sasa na familia yake, ametoa amri ardhi yake mpya iwe kituo cha ukulima. Sasa anavalia nguo za kimalkia na taji yake ya kifalme popote aendapo na anasema ‘inampendeza’ kuwa binti wa mfalme, lakini bado hajafahamu ni lini atakapozuru anachofikiria kuwa nchi mpya zaidi ulimwenguni

Itabidi Misri, Sudan na Umoja wa Mataifa kutambua ‘Ufalme wa Sudan’ kabla hajakuwa rasmi bintiye mfalme.