Jeremy Heaton aliambia BBC kuwa amesafiri kutoka Virginia nchini Marekani na bendera yake kutangaza eneo hilo kwa Ufalme wa ‘Sudan Kaskazini’, eneo hilo ni jangwa la mraba wa maili 800 lililo kati ya Misri na Sudan, na halijamilikiwa na nchi yoyote Alisema kuwa ameandikisha rasmi maombi kwa nchi hizo mbili, japo bado hajapata jibu
Princess Emily akiwa amevaa tiara |
Ili kuadhimisha miaka saba tangu kuzaliwa kwa bintiye, Heaton alisafiri kwenda panapofahamika na wenyeji kama ‘Bir Tawil’ ili kutimiza ombi la Emily
Picha ikionyesha kipande cha ardhi cha Bir Tawil kinachotakiwa na Bwana Jeremy Heaton ili aweze kukitawala kama mfalme wa eneo hilo |
Alidai kuwa kwa miaka mingi nchi kadhaa, ikiwemo Marekani, zilidai umiliki wa ardhi kwa kuweka bendera kwenye ardhi hiyo. Sasa bwana Heaton anasema atajaribu kuomba usaidizi kutoka kwa Umoja wa Afrika (AU)
Mzozo wa mipaka kati ya nchi ya Sudan na Misri unaashiria kuwa jangwa hilo ni kati ya vipande vya mwisho duniani visivyomilikiwa, tofauti, anavyosema, ni kuwa aghalabu vita huzuka ili kupata umiliki huo, bali kwa kesi yake, kuanzisha nchi hiyo ni ishara ya mapenzi yake kwa bintiye
Hata kama hakuna uwezekano kuwa Jeremy Heaton atakuwa mfalme wa nchi hiyo mpya ya Sudan kaskazini, ana mipango atakavyoendeleza nchi hiyo
Binti mfalme Emily, aitwavyo sasa na familia yake, ametoa amri ardhi yake mpya iwe kituo cha ukulima. Sasa anavalia nguo za kimalkia na taji yake ya kifalme popote aendapo na anasema ‘inampendeza’ kuwa binti wa mfalme, lakini bado hajafahamu ni lini atakapozuru anachofikiria kuwa nchi mpya zaidi ulimwenguni
Itabidi Misri, Sudan na Umoja wa Mataifa kutambua ‘Ufalme wa Sudan’ kabla hajakuwa rasmi bintiye mfalme.