Select Menu

Ads

Random Posts

Powered by Blogger.

Design

Technology

Circle Gallery

Shooting

Racing

News

Bottom

Wednesday, August 6, 2014

Michuano ya klabu Bingwa Afrika mashariki na kati maafuru Kagame Cup inaanza Agosti 8 mwaka huu

Kindumbwe ndumbwe cha michuano ya klabu Bingwa Afrika mashariki na kati maafuru Kagame Cup kinaanza kesho ambapo mechi ya ufunguzi ya Kundi A ni kati Atlabara ya Sudan Kusini ambayo itamenya na KMKM ya Zanzibar kuanzia saa saba mchana.

Mechi ya pili itakuwa ni mechi ya kundi B kati ya Gor Mahia ya Kenya ambao watapepetana vikali na KCCA ya Uganda . 

Wenyeji Rayon sports ya Rwanda itashuka dimbani kumenyana na Azam ya Tanzania katika mechi nyingine ya kundi A. 

Azam ya Tanzania imepata nafasi ya kucheza michuano hiyo baada ya Yanga pia ya Tanzania kuondolewa kwa kutotimiza vigezo vya michuano hiyo ambapo ni pamoja na kupeleka kikosi cha pili cha timu hiyo.