Select Menu

Ads

Random Posts

Powered by Blogger.

Design

Technology

Circle Gallery

Shooting

Racing

News

Bottom

Monday, July 21, 2014

Maimartha Jesse ‘Mai’ aamuwa kumsuta mvulana kwa keki yenye maneno yasemayo 'Sajo acha umbea ndoa tamu'

Dume lililofahamika kwa jina moja la Lusajo au Sajo anayefanya kazi maeneo ya Kijitonyama, Dar jirani na duka la mtangazaji Maimartha Jesse ‘Mai’ amejikuta akitaharuki na kuaibika baada ya kusutwa laivu katikati ya wanawake huku akilishwa keki na kufunguliwa mvinyo kisa umbeya.
Mwanaume aliyesutwa akilishwa keki na Maimartha.

Kwa mujibu wa mashuhuda waliokuwa eneo la tukio wikiendi iliyopita kabla ya gazeti hili kutua, Maimartha alidaiwa kusuka ishu hiyo huku akiwakaribisha marafiki zake kushuhudia akiwemo Flora Mvungi.

Ilisemekana kwamba Mai alidai kuwa kilio chake kwa muda mrefu ni kwamba jamaa huyo amekuwa akimfuatafuata na kumwambia mumewe, Raymond Shayo ‘Shaa’ kila jambo analolifanya dukani hapo, ikiwa ni pamoja na kumweleza watu wa kila aina wanaoingia ndani hapo. 
“Nilishapata taarifa za Sajo kuwa huwa ananichunguza, sikutaka kuwa na haraka nikaenda naye taratibu bila kumwambia kwani nilikuwa nikimtafutia dawa ya kumkomesha. Leo ndiyo arobaini yake imefika.

“Nilishika simu ya mume wangu nikakuta SMS za Sajo zikimuomba fedha, ukweli nilichukia sana na nilishangaa kuona kumbe kazi anayoifanya ya kunichunguza analipwa, nikaona sasa ndiyo wakati wa kumkomesha kwani kwa kulipwa kwake ipo siku atatunga hata uongo kwa sababu fedha ni shetani,” alisema.

Keki ya msuto aliyoandaliwa Bw. Sajo.



Sajo, kabla ya kujua kinachoendelea, alikaribishwa keki na shampeini, akaenda kichwakichwa, alipomaliza kulishwa akaambiwa asome maneno yaliyoandikwa kwenye keki ‘Sajo acha umbeya ndoa  tamu’ ndipo akachanganyikiwa na moja kwa moja msuto ukaanza huku akiulizwa ni kwa nini anamwambia maneno mume wa Mai.


“Mh! Mimi mbona siyo kweli jamani,”  alisema Sajo na kushindwa kumalizia maneno. Alipobanwa na wanahabari wetu na Gea Habibu (wa Leo Tena ya Clouds FM) juu ya kuwa na namba ya simu ya mume wa Mai, Sajo alishikwa na kigugumizi na kuondoka ambapo alikimbilia dukani kwake na kujifungia kukwepa aibu kwani siyo tukio la kawaida kwa mwanaume kusutwa kwa umbeya.

Credit GPL