![]() |
Picha hiyo imeshatolewa kwenye mtandao wa Instagram. |
Picha hiyo kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram, ilikuwa na ujumbe unaosema: “busu kwa wote wenye chuki”.
Mchezaji huyo aliyejiunga na AC Milan akitokea Manchester City mwaka 2013, amekuwa katika mizozo na pia kutafutwa na wabaguzi wa rangi.
Hivi karibuni alikosolewa kwa uchezaji wake kwenye Kombe la Dunia. Tukio hilo la picha, halikutiliwa maanani na makamu wa rais wa AC Milan Adriano Galliani aliyedai kuwa kushughulikia suala hilo ni kuingilia haki za mtu binafsi.
Balotelli amekuwa kwenye matatizo kwa miaka kadhaa.
Mwaka 2010, alipiga risasi angani akiwa kwenye mgahawa wa pizza wa Della Republicca wa mjini Milan na 2011 maafisa wa Manchester City walimfanyia uchunguzi baada ya kurusha kimshale kwa mchezaji kinda kwenye uwanja wa mazoezi wa timu hiyo.
liwahi kuripotiwa kuwa Mario alikuwa akikusanya maelfu ya pauni kama faini za maegesho ya magari mjini Manchester, na aliitwa kuhojiwa na kocha Roberto Mancini.