Select Menu

Ads

Random Posts

Powered by Blogger.

Design

Technology

Circle Gallery

Shooting

Racing

News

Bottom

Wednesday, July 9, 2014

Nusu fainali ya pili Brazil, Waholanzi wawakebehi Argentina

Wakati mashabiki wa soka wa nchini Brazil wakiendelea kujiuliza KULIKONI? Vyombo vya habari vya nchini Uholanzi vimeanza mbwembwe kuelekea katika mchezo wa pili wa hatua ya nusu fainali ambapo timu ya taifa ya nchi hiyo itapambana na Argentina. 

Gazeti la De Telegraph la nchini Uholanzi limetoa picha ya kocha wa timu ya taifa ya nchi hiyo ambayo ilimkebehi mchezaji wa FC Barcelona na timu ya taifa ya Argentina Lionel Messi. 

Picha hiyo ya kejeli imeweka katika ukrasa wa mbele wa gazeti hilo, kwa kuashiria Argentina hawana chao kuelekea kwenye mchezo huo ambapo mshindi atakaepatikana ataungana na Ujerumani katika mchezo wa hatua ya fainali uliopangwa kuchezwa siku ya jumapili huko nchini Brazil.

Gazeti lingine la nrc nalo limetoa picha inayomkebehi Lionel Messi, ambaye ni nahodha wa kikosi cha Arngetina ambapo bado picha hizo zinachukuliwa kama ushindi wa vita ya nje ya uwanja. 

Katika gazeti hilo picha ya Lionel Messi inaonekana akiwa anakamua juisi ya machunga ambayo itanywewa na na wachezaji wa timu ya taifa ya Uholanzi mara baada ya mchezo wa hii leo.