Claire Leeson, msichana mwenye umri wa miaka 24, mkaazi wa Landani ametumia zaidi ya $30,000 (Tsh 49,755000)kufanya upasuaji ili afanane na Kim Kardashian.
Claire ameiambia This Morning kuwa aliamua kufanya hivyo kwa sababu alipokuwa shuleni wenzake walikuwa wanamcheka na kuuita ‘mbaya’ kuliko kitu chochote kilicho hai.
“Nilikuwa naambiwa kila siku mimi ndiye mbaya kuliko kitu chochote kilicho hai na kwamba inabidi nijiue. Nilipoacha shule marafiki zangu waliniambia kuwa ninavitu ambavyo vinafanana na Kim Kardashian.” Amesema Claire.
Ameeleza kuwa baada ya kuambiwa hivyo na marafiki zake aliamua kuanza kuangalia kwa makini Keeping Up With The Kardashians na akagundua kuwa kweli kuna vitu ambavyo wanafanana na Kim Kardashian.
“Tunafanana katika mabishano na vitu vingine. Nikafikiri ni mzuri sana na kwa kweli nilitaka kufanana nae.”
Boob Job- $8500Hata hivyo, msichana huyo ambaye kwa kiasi fulani zoezi hilo limemuweka katika madeni amesema anaona alichokifanya kinathamani ya fedha aliyotoa.
Teeth Whitening-$4300
Hair Extensions-$7700
Make-up-$1700
Spray Tans-$1700
Nails-$850
Bum Padding-$600
Shoes and Clothes-$5400