Video Game ya Kim Kardashian imemtajirisha na inaweza kumfanya kuwa miongoni mwa wanawake watatu matajiri zaidi duniani kwenye kiwanda cha burudani kwa mwaka 2014.
Mchambuzi wa Doug Creutz aliimbia Bloomberg kuwa video game hiyo itamuingizia Kim Kardashian kiasi cha $ 200 million, huku ikiwa imeshika nafasi ya kwanza kwenye iTunes na inadaiwa kuwa video game ya kwanza kufikia rate ya nyota 5 mwaka huu.
Mchambuzi huyo ameeleza kuwa umaarufu wa jina la Kim Kardashian limewavutia wengi kudownload application hiyo, lakini kwa sasa game hilo linaendelea kuwa na umaarufu wake.
Tayari video game hiyo imekuza hisa ya kampuni ya Glu Mobile kwa 42%, na Chief Operating Officer wa kampuni hiyo ameeleza kuwa ni video game kubwa zaidi ya mwaka kwao, “Our biggest game of the year.”
Ingawa inapatikana kwa free, lakini inawawezesha watumiaji kununua vitu vya digitali (digital accessories) kwa pesa.
Tuesday, July 15, 2014
Video Game ya Kim Kardashian yavunja rekodi, kumuingizia zaidi ya $200 million
Labels:
Entertainment,
Video