Select Menu

Ads

Random Posts

Powered by Blogger.

Design

Technology

Circle Gallery

Shooting

Racing

News

Bottom

Tuesday, September 23, 2014

Picha za mtindo wa vazi la usiku kwa wanawake

Baadhi wanawake siku hizi wamekuwa wakijiuliza vazi gan ambalo linafaa kuvaliwa wakati wa usiku na likawapendeza sasa unaweza kutazama picha hizi


Wednesday, August 6, 2014

Wiz Kid amjibu Davido kupitia twitter baada ya Davido kusema hakuna Beef

Beef ya mastar wa Nigeria inaonekana bado haijaisha baada ya Davido kuzungumzia kitu gani kilimkasirisha hadi bifu na Wiz Kid kutokea, Wiz ameingia twitter na kumjibu bila kumtaja jina kama kawaida yao. Tweet hiyo inadhihirisha kwamba Wiz Kid hakupenda jinsi Davido alivyozungumza kuhusu hilo beef.


Ile kauli ya Diamond kwamba hawezi kuoa kamwe, yamchefua Wema

KAULI ya nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kwamba hawezi kuoa kamwe, inadaiwa kumchefua mwandani wake, Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’.

Aliporejea Bongo kutoka Marekani juzikati, Diamond alitoa kauli hiyo na kuandikwa kwenye ukurasa wa mbele wa gazeti dada la hili, Ijumaa, toleo la wiki iliyopita likiwa na kichwa cha habari; ‘DIAMOND: SITAOA KAMWE’ ambapo ndani yake alieleza jinsi ambavyo mastaa wengi waliooa wameanguka kisanii.

Kwa mujibu wa mtu wa karibu wa mastaa hao, Wema hakufurahishwa na habari hiyo kwa sababu anajua yeye ndiye mke mtarajiwa wa Diamond. 
Ilidaiwa kwamba, Wema alijikuta akipoteza ile furaha ya kwamba wawili hao wangefunga ndoa mwezi huu (Agosti) kama ilivyotabiriwa na mnajimu maarufu Bongo, Maalim Hassan Yahya Hussein. 

“Baada ya kauli hiyo ya Diamond na kutotimia kwa utabiri wa Maalim Hassan kwa sababu hakuna hata dalili za maandalizi ya tukio hilo muhimu kwenye maisha ya mwanadamu, Wema ameanza kukata tamaa, lakini amesema hawezi kulazimisha ndoa kwa mwanaume kwa kuwa si utamaduni wa wanawake wa Kitanzania wala Kiafrika.

“Unajua Kibongobongo au hata Kiafrika hai-sound vizuri na pengine haiwezekani kwa mwanamke kulazimisha kuolewa kama mwanaume hataki. Hicho ndicho kilichomtibua Madam (Wema) baada ya kusoma alichokisema Diamond,” kilisema chanzo hicho na kuongeza: 

“Wema amehisi yeye ni girl lover (mpenzi) tu kwa Diamond na si wife material (mke mwema) kwa hiyo  anawaza sana kuhusiana na ishu hiyo japo mahaba niue kati yao yanaendelea, lakini anafikiria kuchukua uamuzi mzito.”

Baada ya kuinyaka ishu hiyo, gazeti hili lilimtafuta mlimbwende huyo anayeshikilia Krauni ya Miss Tanzania 2006 ili kumsikia mwenyewe ambapo alifunguka yake ya moyoni. Mwanadada huyo alisema kuwa kwa sasa haumizi tena kichwa kuhusu  suala la ndoa na Diamond na kwamba hana haraka nalo. 
“Mimi naamini sana mambo ya utabiri, lakini siumizi kichwa na suala la kuolewa na Diamond na kamwe siwezi kumlazimisha anioe.

“Kikubwa katika mapenzi ni upendo wa kweli ambao ananionesha bila kipimo. Wala sina papara, hata kama mtabiri kasema ndoa yetu ni lazima ifungwe mwaka unaogawanyika kwa mbili kwa maana ya mwaka 2016 kama itashindikana mwezi huu, hilo kwangu si tatizo la kunifanya nililie kuolewa na Chibu (Diamond). 

“Ninachojua mimi Mungu ndiye anapanga yote na kama ndoa ipo ipo tu maana kuna watu wapo kwenye ndoa na hawana upendo wa kweli kama tulionano sisi,” alisema Wema.

Paparazi wetu alimtwangia simu mama yake Wema, Mariam Sepetu na kumuuliza mambo mawili, kuhusu bintiye kuvishwa pete ya ndoa na Diamond na suala la Mbongo Fleva huyo kusema hataoa kamwe!
“Mimi niseme nini? Sina la kusema kuhusu Wema. Mambo yake ni yake mwenyewe na huyo Diamond wake. Kwanza kwa nini mnipigie mimi, si mumtafute yeye mwenyewe?” alisema mama huyo kwa sauti ya utulivu.

Katika hali ya kushangaza, mama Diamond, Sanura Kasim ‘Sandra’ ameonekana kunawa mikono kwa kauli aliyowahi kuitoa siku za nyuma kuhusu mtoto wake na masuala ya kutooa au kuoa. 
Nasibu ni mtu mzima sasa, siwezi kumpangia lolote kuhusu kuoa au kutooa. Wakati ukifika, anaweza kusema lolote ambalo ataliona ni zuri katika maisha yake.”

Kuhusu Diamond kumvisha pete ya ndoa Wema, tendo ambalo lilifanyika hivi karibuni wakiwa nchini Afrika Kusini, Amani lilifanikiwa kuzungumza na shehe mmoja ambaye aliomba hifadhi ya jina lake ambapo alisema alichokifanya Diamond kwa Wema ni usanii. 

“Diamond amemfanyia usanii mwenzake. Pete gani bila kufunga ndoa. Halafu katika Uislam, hakuna tendo la wanandoa kuvalishana pete, hayo mambo wanayafanya wenyewe, ” alisema shehe huyo.

Wema alipopewa nafasi ya kuizungumzia pete hiyo alisema Diamond aliipenda tu akaamua kumnunulia na kumvisha lakini haihusiani na ndoa. 

“Sisi (na Diamond) tulikuwa Afrika Kusini, baby wangu akaipenda pete, akainunua na kunivalisha, haina uhusiano na ndoa,” alisema Wema.

Credit GPL.

Michuano ya klabu Bingwa Afrika mashariki na kati maafuru Kagame Cup inaanza Agosti 8 mwaka huu

Kindumbwe ndumbwe cha michuano ya klabu Bingwa Afrika mashariki na kati maafuru Kagame Cup kinaanza kesho ambapo mechi ya ufunguzi ya Kundi A ni kati Atlabara ya Sudan Kusini ambayo itamenya na KMKM ya Zanzibar kuanzia saa saba mchana.

Mechi ya pili itakuwa ni mechi ya kundi B kati ya Gor Mahia ya Kenya ambao watapepetana vikali na KCCA ya Uganda . 

Wenyeji Rayon sports ya Rwanda itashuka dimbani kumenyana na Azam ya Tanzania katika mechi nyingine ya kundi A. 

Azam ya Tanzania imepata nafasi ya kucheza michuano hiyo baada ya Yanga pia ya Tanzania kuondolewa kwa kutotimiza vigezo vya michuano hiyo ambapo ni pamoja na kupeleka kikosi cha pili cha timu hiyo.

Kim Kardashian abadili jina lake kisheria, aonesha kwenye passport

Siku 74 baada ya kufunga ndoa na Kanye West huko Florence, Italia Kim Kardashian amefuata taratibu za kisheria na kubadili jina lake rasmi kwa kuweka jina la Kanye West. 
Mwanamitindo huyo amefanya mabadiliko hayo na kushare kwenye Instagram Jumanne, July 5. “New passport pic #Mrs.West #NameChange.” 

Kim Kardashian amekuwa atumia jina la Kim Kardashian West kwenye Instagram lakini halikuwa jina lake rasmi kisheria, hadi jana alipofanya mabadiliko na kulihamishia kwenye passport yake na kila kitu kinachomtambulisha kisheria.

Kesi nzito yafunguliwa tena dhidi ya Michael Jackson, mlalamikaji atoa ushahidi wa kulawitiwa utotoni

Wakati Michael Jackson akiwa amelala kwenye nyumba yake ya milele, bado familia yake imeendelea kuandamwa na tuhuma nzito zinazomhusu mfalme huyo wa Pop duniani. 
Mlalamikaji, James Safechuck mwenye umri wa miaka 36 hivi sasa ambaye alikuwa katika kesi ya Michael Jackson ya mwaka 2005 kuhusu ulawiti, ameibuka tena na kufungua kesi na kutoa ushahidi mpya wa jinsi alivyokuwa akilawitiwa na marehemu mwaka 1988 wakati akiwa mtoto mwenye umri wa miaka 10 tu.

James ambaye sasa ni baba wa familia hakuonesha ushirikiano wakati wa kesi ya mwaka 2005 licha ya kutajwa kama sehemu ya ushahidi. 

TMZ wameeleza kuwa wamepata nyaraka zilizowasilishwa na Safechuck mahakamani ambazo zinaeleza kuwa Michael Jackson alimfundisha lugha ya ishara wakati akiwa na umri wa miaka kumi, lugha ambayo alikuwa akiitumia kutaka kumueleza kuwa anataka kufanya nae mapenzi. 

Ameeleza kuwa moja kati ya ishara hizo ni pale walipokuwa wakishikana mikono kusalimiana, alikuwa anambinya au kumtekenya katikati ya kiganja. 

Katika nyaraka hizo ameendelea kueleza kuwa MJ alikuwa anamchukua na kumpeleka kwenye majumba ikiwa ni pamoja na sehemu inayoitwa ‘The Hideout’ ambapo walikuwa wakinywa vinywaji laini, pink wine na kuangalia video za ngono. 
Amesema marehemu aliendelea kumfanyia vitendo hivyo  hadi pale alipoanza kubalehe. 

Hata hivyo, mwanasheria wa Michael Jackson, Howard Weitzman ameiambia TMZ kuwa kesi hiyo inatakiwa kutupiliwa mbali kwa kuwa imeletwa kwa mara ya kwanza miaka 20 baada ya tukio hilo analolieza na kwamba James Safechuck aliwahi kula kiapo na kueleza kuwa Michael Jackson hakumfanyia kitu chochote kibaya.

Audio: Linex atangaza nia ya kugombea ubunge 2020 kupitia chama kipya

Baadhi ya Mastar wa Tanzania wameamua kuweka wazi nia zao za kugombea nafasi za uongozi katika ngazi mbalimbali,miongoni mwa watu hao kwa sasa ni msanii kutoka Kigoma All Stars anaitwa Linex Mjeda.

Amekua wazi kutaja chama ambacho anategemea kugombania nafasi yake ya ubunge aliyosema kuwa tayari ana jimbo anasubiri muda tu na chama alichosema anategemea kugombea ni chama kipya cha ACT.

Soudy Brown amemuuliza maswali mengi ikiwemo kama kweli ana kadi ya chama,sikiliza alichojibu hapa.

Bonyeza play kusikiliza.