Select Menu

Ads

Random Posts

Powered by Blogger.

Design

Technology

Circle Gallery

Shooting

Racing

News

Bottom

Friday, July 11, 2014

Dayna ajipanga kutoa kichupa

Msanii wa muziki nchini Dayna Nyange
Msanii wa kike ambaye anakubalika sana katika muziki wa kizazi kipya nchini Dayna Nyange anatarajia kutoa video ya wimbo wake mpya ambao unatarajiwa kukamilika baada ya mwezi huu mtukufu wa Ramadhan.

Dayna ambaye kwa sasa anafanya poa na wimbo wake 'I Do' ameiambia enewz kuwa kwanza anatoa shukrani zake za dhati kwa mashabiki wake kuupokea vyema wimbo wake huo na amewasihi wategemee shooting kali ya wimbo huo. 

Dashosti huyo amesema kuwa hii itakuwa ni surprise kubwa sana kwani katika video hiyo mpya amejitahidi kubadilika tofauti na video zake zote alizowahi kufanya hapo awali, ambapo prodyuza mahiri anayeipika kazi hiyo ni Triss kutoka studio maarufu ya Conga Music jijini Dar es Salaam. 
Dayna pia ametuma picha zake za kuwatakia mashabiki wake wote mfungo mwema wa mwezi huu mtukufu wa Ramadhani .