Select Menu

Ads

Random Posts

Powered by Blogger.

Design

Technology

Circle Gallery

Shooting

Racing

News

Bottom

Friday, July 11, 2014

Neymar aeleza mkasa mzima, amuunga mkono Messi

Kabla yakufanya mahojiano na waandishi wa habari, Neymar, 22, katika hali ya majonzi alikwenda kuwasalimia wachezaji pamoja makocha wa timu yao ya taifa wakati wakifanya mazoezi katika kambi yao kwa ajili ya kujianda na mchezo wa kumtafuta mshindi wa tatu dhidi ya Uholanzi, mchezo utakaochezwa siku ya Jumamosi. 

Katika mahojiano hayo Neymar alizungumzia juu ya kuombwa msamaha na mlinzi wa Colombia aliyemsababisha akose mechi yao ya nusu fainali dhidi ya Ujerumani. 

“Carlos Zuniga alinipigia simu na kuniomba msamaha na nikakubali,  sidhani kama alikuwa amedhamiria kuniumiza lakini kwa watu wanaojua mpira wa miguu nadhani ile haikuwa rafuu ya kawaida”, alieleza Neymar. 

Inasemekana kwamba Neymar alizima televisheni yake mara baada ya Ujerumani kufunga goli la saba, katika mchezo huo ambao uliishia kwa magoli 7-1.  “Nilihisi kuchanganyikiwa na kutoamini kilicho tokea”, alisikika Neymar  Pia aligusia mchezo wa fainali ambapo watani wao wa jadi Argentina watacheza na Ujerumani. 

“Mimi sio shabiki wa Argentina ila nataka wachezaji wenzangu wa Barcelona Messi na Mascherano wachukue Kombe la Dunia, timu yangu ni Messi football club.”