Select Menu

Ads

Random Posts

Powered by Blogger.

Design

Technology

Circle Gallery

Shooting

Racing

News

Bottom

Monday, July 14, 2014

Kigali wakubali kazi na Cindy

Baada ya taarifa kutoka kwa msanii Cindy wa Uganda kuelezea nia ya kufanya kolabo na kundi nyota la nchini Rwanda-Kigali, tayari kundi hilo limeweka taarifa wazi kwa mashabiki wao kuwa wamekubali kufanya nae kazi.
kundi la Urban Boys nchini Rwanda
Kundi hilo linalofanya miondoko ya Afro-Beat limekubali kufanya kolabo na Cindy baada ya mwanadada huyo kulifagilia kundi hilo baada kutumbuiza vyema hivi karibuni katika sherehe za siku ya ukombozi zilizofanyika hivi karibuni nchini Rwanda. 
Cindy Sanyu

Mmoja wa memba wa kundi hilo Humble Gizzo ameelezea kuwa wanashukuru kupata sapoti yake kwani kufanya nae kazi itawasaidia kuukuza muziki wao zaidi ndani ya nchi za Afrika Mashariki.