Select Menu

Ads

Random Posts

Powered by Blogger.

Design

Technology

Circle Gallery

Shooting

Racing

News

Bottom

Friday, July 4, 2014

Rais Mugabe awafukuza wakulima wote wazungu Zimbabwe

Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe ameurejea uamuzi alioufanya miaka mingi iliyopita wa kuwafukuza wakulima wa kizungu nchini humo, na sasa amekaza kamba zaidi.  Mugabe ametoa tamko katika mkutano wa hadhara kuwa hawataki wakulima wa kizungu na kwamba ni lazima waondoke. 
Hatuwataki wakulima wazungu kumiliki mashamba yetu, lazima waondoke.” Rais Mugabe anakaririwa. 

Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe, amewataka wakulima wazungu waliosalia nchini humo kuondoka na kuwaachia mashamba wazalendo wa nchi hiyo. 

"hatuwataki wakulima wazungu, kumiliki mashamba yetu, lazima waondoke,'' Mugabe aliwaambia wafuasi wake katika mkutano wa hadhara. 

Rais Mugabe ameendelea kushikilia msimamo wa kuwapokonya ardhi wazungu na kuwamilikisha raia wa nchi hiyo huku akitaka wazawa kutokuwa wakarimu sana kwa wazungu kwa kuwa mashamba sio yao. 

Mugabe mwenye umri wa miaka 90 ameiongoza Zimbabwe tangu ipate uhuru mwaka 1980 na mwaka jana alishinda katika uchaguzi mkuu wa nchi hiyo kwa kupata asilimia 61 ya kura zote zilizopigwa.