Select Menu

Ads

Random Posts

Powered by Blogger.

Design

Technology

Circle Gallery

Shooting

Racing

News

Bottom

Friday, July 4, 2014

Wasichana waliotekwa na Boko Haram hubakwa wakichukuliwa video

Wasichana zaidi ya 200 wa Chibok waliotekwa na kundi la Boko Haram wanadaiwa kuwa katika hali mbaya na ya kutisha zaidi senator wa jimbo la Borno anasema hufanyiwa vitendo vya kinyama kupita maelezo. 
Akifanya mahojiano na kituo cha runinga cha Sahara TV, Senator Khalifa Ahmed Zanna wa Borno Central amesema amepata ripoti mpya kuwa wasichana hao waliotekwa siku zaidi ya 70 zilizopita hubakwa na wafuasi wa kundi hilo huku wakichukuliwa video ambayo baadae huoneshwa hadharani. 

Senator huyo ameeleza kuwa ingawa hakushuhudia video hiyo lakini mtu aliyemsimulia matukio hayo alikuwa na video hiyo na alieleza kuwa msichana akimaliza kubakwa hupiga magoti mbele ya mbakaji na kumuomba amhurumie. 

Therefore the girl after being raped, she curled down to the man, kneeling down and begging him to please be patient. So disturbing. And although I didn’t see the video, the person narrated to me, he said he had the video, and he was narrating to me, and look at the situation.” Amesema Senator Khalifa. 

Amesema mbali na wasichana hao waliotekwa, kundi hilo limewakamata wanawake zaidi ya 500 wanaokutwa barabarani au vijijini. 

Mbali na tukio hilo la kinyama, amesema ripoti aliyopewa inaonesha kuwa kundi hilo hivi sasa halina chakula cha kutoshwa hivyo linaingia vijijini na kuwanyang’anya wanakijiji chakula walichonacho huku wakifanya matukio ya kinyama. 

Kufuatiak matukio hayo wanakijiji wengi wamekimbia makazi yao na kuhamia mijini bila kujua hatima yao huku wengine wakiingia kwenye nchi za jirani.